1. Ndugu wa kirohoni
Mliokombolewa,
Tafakarini sana
Yatupasayo.
Wapenzi wake Yesu
Tuliokombolewa
Tujitoe kabisa
Wengi waponywe.
2. Siku itatimia
Tutakapoulizwa
Wale wa nyumba zetu
Na majirani
3. Tujitoeni, ndugu,
Tukahubiri Injili.
Atutumie Roho
kuponya wengi.
4. Wasiokombolewa
Ni wengi vijijini,
Wataokolewaje
Tukiogopa?
5. Bwana alijitoa
Akapotewa mengi,
Ili atuokoe,
Tusiwe waoga.
6. Aliyetununua,
Kwa kuimwaga damu,
Angalieni sana
Msimwepuke.