Return to Index

135

136

Msifuni Yesu ndiye mkombozi;

137
SongInstrumental
	

1. Msifuni ,Yesu ndiye mkombozi; Imbeni ya pendo zake kuu, Sujuduni,malaika mlioko, Jina lake liwe na sifa kuu. Kama vile mchunga uchungavyo Vivyo sisi kutwa atachunga. Msifuni mlio wake watoto Msifuni aliye mchunga. 2. Msifuni,Yesu ndiye mkombozi; Akateswa tupate ongoka; Ndiye Mwamba,Dhamana ya kuokoka; Sujuduni kwake muangikwa, Yesu aliyeudhiwa na hamu Kwa pendo za baba yake Mungu. Aliyefyolewa na kusulubiwa. Msifuni ndilo letu fungu. 3. Msifuni,Yesu ndiye Mkombozi; Shindukeni,enyi malango juu; Bwana Yesu tangu milele Mwokozi, Mvikeni taji, ni yake tu. Atakuja kuitawala nchi, Yesu,Mwombezi wetu wa Mungu. Msifuni, ni mfalme wa salama; Ndiye kweli mwana wake Mungu.