Return to Index
155 |
156
Bwana Yesu yuko wapi
|
157 |
Song | Instrumental |
|
|
1. Bwana Yesu yuko wapi,
Mpenzi wangu rafiki?
Njia gani amekwenda?
Nitamwonaje mimi?
Roho yangu yajutishwa
Na dhambi na huzuni;
Yesu mpenzi wangu Mwema
Namtafuta kwa bidii.
2. Ninapaza sauti yangu
Nalia:wapi Yesu?
Ndani mwangu sina raha
Mpaka nimwone Yesu.
Ningekuwa na mabawa
Ningeruka upesi
Milimani, mabondeni
Kumtafuta Bwanangu
3. Aondoa shida zangu,
Maharibifu yote.
Nikiona taabu mimi
Anituliza yeye.
Nitafanya bidii sana;
Kumtafuta popote;
Sitachoka kutembea
Mchana hata usiku.
4. Bwana Yesu nitokee,
Roho inakuita.
Niondoe na maovu
Yesu mwokozi wangu.
Utilize hamu yangu
Kaa kwangu daima.
Nikupende sana wewe,
Niwe wako milele.