1. Jioni moyo wangu
wakutafuta Bwana,
na kukushukuru.
Unikazie macho
yenye baraka nyingi,
ung’aze mwili na roho.
2. Natumaini tena
rehema yako Baba
hata usiku huu.
Fukuza majaribu
na hila ya shetani,
ukiwa karibu yangu
3. Unanipenda sana,
wakaa pamoja nami,
wanikaribisha.
Unanifurahisha
kwa wema wako
mwingi,
sababu hii nakusifu.
4. Maisha yanapita upesi,
ni safari ya kwenda
mbinguni.
Unifundishe, Bwana,
kuelekea kwako:
Pazuri ni mbinguni tu.