Return to Index

38

39

Mwenye dhambi huna raha

40
SongInstrumental
	

1. Mwenye dhambi huna raha, Sikiza nakusihi, Utapata msamaha Kwake Yesu Mwokozi! Njoo hima, njoo hima, Naye atafurahi. 2. Yesu anakwita sana Naye yuko Mbinguni; Hofu ya kifo hapana Kwake ukiamini. Njoo hima, njoo hima, Utapata amani. 3. Hatakwita siku zote; Ni ya sasa nafasi. Lete na uchafu wote, Kukawa haipasi. Njoo hima, njoo hima, Ni wokovu halisi. 4. Uzima uko kwa Bwana Twae uzima hasa Bure unapatikana, Wokovu twae sasa! Njoo hima, njoo hima, Twae utakatifu.