Return to Index

4

5

Jina lake Yesu tamu;

6
SongInstrumental
	

1. Jina lake Yesu tamu; Tukilisikia Hutupoza, tena hamu Hutuondolea. 2. Roho iliyoumia Kwalo hutibika, Chakula, njaani pia; Raha, tukichoka. 3. Jina hili ni msingi, Ngao, ngome, mwamba, Kwa hili napata wingi, Kwangu ni akiba. 4. Yesu, Mchunga, Rafiki Mwalimu, Kuhani, Mwanzo, Mwisho, Njia, Haki, Uzima kifoni. 5. Moyo wangu hauwezi, Kukusifu kweli, Ila sifa zangu hizi, Bwana zikubali. 6. Na utakaponiita, Kuja kwako Bwana, Huko kwako sitaacha Kukusifu sana.