1. Chini ya msalaba
Nataka simama;
Ndio mwamba safarini,
Wa kivuli chema;
Ni kweli kwa roho yangu
Ni tuo kamili,
Tatua mzigo wangu
Wakati wa hari.
2. Hapa ni pema sana,
Ni ngome kamili;
Hapa yameonekana,
Mapenzi ya kweli;
Kama alivyoonyeshwa
Yakobo zamani,
Msalaba umekuwa
Ngazi ya Mbinguni.
3. Na Yesu msalabani
Walimkemea,
Alikufa niokoke
Niliyepotea;
Naona ajabu sana
Ya mambo mawili
Jinsi alivyonipenda,
Nisiyestahili.
4. Atakayeonana,
Na Yesu Mbinguni,
Njia yake aanzapo
Ni msalabani;
Wokovu upo hapa tu,
Mwingine hapana,
Kisha kuna furaha kuu
Pamoja na Bwana.