Return to Index
87 |
88
Ndiyo damu ya baraka ituoshayo
|
89 |
Song | Instrumental |
|
|
1. Ndiyo damu ya baraka ituoshayo wakosa,
Kwake Bwana twaokoka, nasi twamsifu sasa;
Nimestahili hukumu, siwezi kujitakasa;
Nioshe katika damu, takuwa safi kabisa.
Safi kabisa; safi kabisa!
Nioshe katika damu;
Takuwa safi kabisa.
2. Yesu alivikwa miiba, na kuangikwa Mtini,
Na maumivu si haba yaliyompata chini.
Nataka kijito hicho niende kuoga sasa;
Ndicho kinitakasacho, nami ni safi kabisa.
Safi kabisa; safi kabisa!
Ndicho kinitakasacho,
Nami ni safi kabisa.
3. Baba, kweli nimekosa, moyo wangu ni dhaifu;
Dhambi ni nyingi kabisa, nipate wapi wokovu?
Yesu kijitoni pako, naja naamini sasa;
Nioshe kwa damu yako, takuwa safi kabisa.
Safi kabisa; safi kabisa!
Nioshe kwa damu yako,
Nami ni safi kabisa.