1. Tegemea mpaka kufa,
Utapata wokovu.
Bwana Yesu ni Mwokozi
Yeye anakupenda.
Uje kwake ‘sikawie’.
Yeye akuokoa.
Njoo upesi! Njoo upesi!
Fika kwa Bwana Yesu.
2. Acha mambo ya dunia
Yakuhangaishayo.
Iko mali ya uzima
Unaitiwaa hiyo.
Mali hiyo ni uzima
Utapewa na Bwana.
Njoo upesi! …
3. Wakatae, waepuke
Wanaokudanganya;
Na wajinga, wakuponza,
Wakupoteza wewe.
Ila wewe ukatae
Kuondoka kwa Yesu.
Njoo upesi! …
4. Ukijua jambo hilo
Usipolifuata
Kosa hilo kubwa sana,
Wapasiwa hukumu.
Vumilia, jizuie
Utapata uzima.
Njoo upesi! …
5. Bwana Yesu amekwisha
Kukutengenezea
Kitu chema kwake Mungu,
Ndiko unakokwenda.
Kile kitu upendacho
Kule utakipewa.
Njoo upesi! …