1. Ondokeni! tunaitwa
na walinzi wa juu mnarani
Yerusalemu, amka wee!
Ni usiku wa manane,
yuaja Bwana wa arusi,
wanawali wako wapi?
Amkeni upesi!
Kaziwasheni taa.
Haleluya!
Fuateni arusini
kwenda kumpokea Bwana!
2. Sayuni anasikia,
moyo waruka kwa furaha,
yu macho anaondoka.
Mponya wake anashuka
mbinguni mwenye
utukufu,
aleta mwanga wa kweli,
taji yake yaja
na Mwana wa Mungu.
Hosiana!
Twafuata kwenye shangwe
tukale karamu yake.
3. Waimbiwa nyimbo nzuri
kwa misemo ya watu wote
na ya malaika mbinguni.
Tukifika mjini kwako
kwenye milango ya malulu
tutakuimbia nasi.
Furaha kama hii
haijasikiwa duniani.
Nasi sasa tunaimba,
tunakusifu, Ee Bwana.