1. Haya, umati wa Yesu,
Ulioungwa naye!
Haya, enendeni hima
Katika vita kubwa!
Shetani tayari,
Kupigana na sisi!
2. Tumfuate Yesu Kristo,
Tumwamini yeye tu.
Mwovu akituvizia
Sisi hatuogopi.
Majeshi ya mbingu
Ni pamoja na sisi!
3. Tukikesha na kuomba
Yesu anayotaka,
Tukishika neno lake
Na kumtegemea
Kwa nguvu hizi tu
Tutaweza kushinda!
4. Sasa haya wenzi wangu,
Tumfuate Yesu tu!
Siku za maisha yetu,
Tuwe katika yeye.
Tuache dunia
Kuingia mbinguni!
5. Pale Mungu atawapa
Taji walioshinda,
Wapate urithi wao
Nyumbani mwa milele.
Hayani! Tuimbe,
Tumsifu Bwana wetu!