1. Haya ee moyo wangu,
imba kwa furaha.
Umwimbie Muumbaji
mbingu na dunia.
Atukuzwaye pote
umsifu na wewe
kwa nguvu zako zote,
umri wako wote.
2. Mungu wake Yakobo.
ndiye Mungu wwetu.
Ukimchagua yeye,
una fungu jema,
unacho kitu chema,
umepata mali;
moyo utakung’aa
shida zitakwisha.
3. Ni mwenye nguvu nyingi,
hana amshindaye,
kwa hekima aumba
vyote ni ajabu,
misitu na mabonde,
milima,mashamba,
vilivyo baharini
wanyama porini.
4. Ana mizungu mingi,
kuponya wanawe.
Anawapa riziki,
hata siku za njaa.
Wenye chakula haba
wanenepa miili:
hata waliofungwa
anawafungua.
5. Mashangilio yote
hayamtoshi yeye.
Ni mwema peke yake
nami ni vumbi tu!
Ananihurumia
kwa kuwa ni wake,
kwa hiyo nalikuza
Jina lake pote.