1. Baba yetu aliye Mbinguni
Amenifurahisha yakini
Kuniambia mwake chuoni
Ya kuwa nami Yesu pendoni.
Anipenda Mwokozi Yesu,
Anipenda, anipenda;
Anipenda Mwokozi Yesu,
Anipenda mimi.
2. Nimuachapo kutanga mbali,
Yeye yu vivyo, hupenda kweli,
Hunirejeza kwake moyoni;
Kweli yu nami Yesu pendoni.
3. Anipenda! Nami nampenda;
Kwa wokovu alionitenda;
Akanifia Msalabani
Kwa kuwa nami Yesu pendoni.
4. Haya kujua yanipa raha;
Kumuamini kuna furaha;
Humfukuza mara shetani,
Kwona yu nami Yesu Pendoni.
5. Sifa ni nyingi asifiwazo,
Moja ni sana katika hizo,
Wala siachi, hata Mbinguni,
Kwimba, “Yu nami Yesu pendoni”.