1. Yesu aliniita, “njoo,
Raha iko kwangu,
Kichwa chako ukilaze
Kifuani mwangu.”
Nilikwenda kwake mara,
Sana nilichoka;
Nikapata kwake raha,
Na furaha tena.
2. Yesu aliniita, “njoo,
Kwangu kuna maji,
Maji ya uzima, bure,
Unywe uwe hai, ”
Nilikwenda kwake mara
Na maji nikanywa:
Naishi kwake, na kiu
Kamwe sina tena.
3. Yesu aliniita, “njoo,
Dunia ni giza,
Ukinitazama nuru
Takung’arizia.”
Nilikwenda kwake mara
Yeye jua langu,
Ni kila wakati mwanga
Safarini mwangu.