1. Peleleza ndani yangu,
Iwe safi nia,
Kwangu kama kwako Mungu,
Idhihiri pia.
2. Peleleza moyo wangu
Uunifunulie,
Yaliyomo ndani yangu
Nami niyajue.
3. Kwanza washe zako tambi,
Kumefunga giza;
Nijue ambavyo dhambi
Ni la kuchukiza.
4. Peleleza na mawazo
Ni mbegu za mambo,
Asili ya machukizo,
Maumbuo – umbo.
5. Zidi kuyapeleleza
Katikati yangu
Hata wishe nifundisha
Udhaifu wangu.
6. Hapo nikikwinamia
Mbele zako, Mungu,
Hakika nitakujua
U mpenzi wangu.