Return to Index

58

59

Peleleza ndani yangu

60
SongInstrumental
	

1. Peleleza ndani yangu, Iwe safi nia, Kwangu kama kwako Mungu, Idhihiri pia. 2. Peleleza moyo wangu Uunifunulie, Yaliyomo ndani yangu Nami niyajue. 3. Kwanza washe zako tambi, Kumefunga giza; Nijue ambavyo dhambi Ni la kuchukiza. 4. Peleleza na mawazo Ni mbegu za mambo, Asili ya machukizo, Maumbuo – umbo. 5. Zidi kuyapeleleza Katikati yangu Hata wishe nifundisha Udhaifu wangu. 6. Hapo nikikwinamia Mbele zako, Mungu, Hakika nitakujua U mpenzi wangu.